Home » , » UGANDA YAFUTA SHERIA DHIDI YA USHOGA, NA USAGAJI.

UGANDA YAFUTA SHERIA DHIDI YA USHOGA, NA USAGAJI.

Written By mahamoud on Friday, 1 August 2014 | 09:06

Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda.

NA BBC SWAHIL.

Mahakama ya kikatiba nchini Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ambayo ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Kadhalika sheria hiyo ilizua gumzo sana, sio tu Uganda bali kote duniani ambapo mataifa ya Magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.
Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja.

Vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, tayari vilikuwa vimeharamishwa Uganda , lakini sheria hiyo mpya pia iliharamisha hatua zozote za kueneza mapenzi ya jinsia moja na wakati huu hata kuwajumuisha wanawake wasagaji kama sehemu ya wapenzi wa jinsia moja.
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.

Share this article :

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2015. Habarika 24 Dev - All Rights Reserved
Customized by Bongotech